Kizazi cha Dawa | Ep 01

0
Simon alikuwa na mke wake ambaye licha ya maisha magumu sana lakini walipendana sana lakini walikuwa na tatizo la kutokuwa na mtoto

Simon na mkewe walikuwa na tamaa sana ya kuwa na mtoto lakini hawakujaaliwa kabisa kumpata

Leo waliwaza jinsi gani wapate mtoto na mawazo makuu ikawa ni kwenda kwa mtaalamu ili wakapewe tiba na suluhisho la kupata mtoto
Hii Simon alifanya bila kumshirikisha mkewe moja kwa moja japo naye baada ya kugundua hakuwa na kipingamizi chochote

Walifika kwa mganga na kuelezea shida zao na mganga akaahidi kuwasaidia huku akiwapa masharti na wakakubali kuwa wangeweza kuyatimiza

Upande mwingine tutakutana na majini yakicheka kwa furaha na kuonesha kuna jambo zuri kwao limetokea na cha kushangaza ni yule mganga ni miongoni mwao na ndiye alikuwa akishangiliwa kwa ujio wake duniani

Baada ya kutoka kwa mganga mke wa Simon alinasa ujauzito na dalili za mwanzo zikaonesha

Baada ya kipindi fulani muda ulifika wa mke wa Simon kujifungua na akajifungua mtoto salama

Maisha yaliendelea kama kawaida na bila kujua chochote Simon alikutana na viatu ambavyo ndani ya filamu utaona aliyeviacha hivyo akavichukua kwani hakuona nani ameviacha pale

Simon alikuwa akijishughulisha na kilimo hivyo alikuwa anapambana kulima mashamba ya watu ili ajipatie kipato hivyo alifanya hivyo ili apate pesa za kulisha familia yake

Sasa mauza uza yanaanza baada ya utulivu wa muda wote na ningependa ujionee mwenyewe mkasa mzima

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)